Muimbaji wa kundi la Chamber Squad, Maze B, amefariki leo saa nne asubuhi, kwa mujibu wa mtu aliyekuwa akimuuguza. 
 
Msanii huyo aliyewahi kufanya vyema na wimbo wake ‘Fikiria’ alikuwa amelazwa katika  hospitali ya Mwananchi mjini Dodoma.

Mez B aliyezaliwa kwa jina la Moses Bushagama alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa Pneumonia.
 
Hivi karibuni aliongea na na kusema kuwa
 
“Nilikuwa na tatizo la Pneumonia tokea mwezi wa 12 nikawa nipo vizuri nilivyo kuja tena Dodoma hali ikabadilika ndo nipo hospitali nimelazwa nasumbuliwa na maumivu ya kichwa na shingo,” alisema.
 
“Nategemea kuruhusiwa muda wowote na sasa hivi naendelea vizuri.” 
 
Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi.

Facebook Blogger Plugin by AllyTz

Post a Comment

 
Top