Kwa mujibuwa mtandao wa  JF, Mwigizaji  wa vichekesho Lucas Mhuvile, almaarufu kama Joti, anayepiga kazi kwenye kampuni ya Orijino Komedi, amemvisha pete mpenzi wake wa ...... siku nyingi, ikiwa ni ishara na dalili njema kwamba safari ya kuelekea kwenye taasisi muhimu zaidi duniani ya NDOA imewadia..


Akiwa na swahiba wake wa siku nyingi, Mr. Mjuni Sylvatory a.k.a Mpoki, Joti alionekana mwenye furaha muda wote kwa kutimiza tendo hilo huku akiwa amealika watu wachache sana kuhudhuria tukio hilo.



Kama ni kweli, tunampongeza sana na kumtakia kila la kheri yeye pamoja na mwenza wake

Facebook Blogger Plugin by AllyTz

Post a Comment

 
Top