Akitoa
taarifa ya mwenyekiti Bungeni wakati wa kuahirisha kikao cha 8 cha
mkutano 18 wa bunge jana, mwenyekiti wa Bunge Mussa Azzan alisema kuwa
Serikali imeridhia kutoa fedha kwa kadri ya mahitaji ya tume ya taifa ya
uchaguzi inayosimamia zoezi hilo.
Maamuzi hayo yalitokana na hoja ya mbunge James Mbatia aliyetaka bunge liahirishe shughuli zake ili kujadili suala hilo kama jambo muhimu na la dharura.
Azzan alisema Kamati ya Uongozi ilikutana katika kikao cha pamoja na serikali pamoja na baadhi ya wabunge akiwemo James Mbatia na kukubaliana kwamba Tume ya Uchaguzi ikutane na Wadau wa zoezi hilo wiki ijayo wakiwemo Kituo cha Demokrasia Tanzania TCD kwa ajili ya kupata suluhu ya mchakato huo.
Alisema pia kuwa katika kikao hicho, kamati ya uongozi imeridhika na maelezo ya serikali kuhusu suala hilo na kuiagiza kamati ya Bunge ya Katiba Sheria na Utawala kulifuatilia suala hilo na kupeleka taarifa bungeni siku ya Ijumaa (Februari 6, 2015).
Hata hivyo taarifa hiyo ya mwenyekiti wa Bunge Musa Azzan haikusema ni kiasi gani na lini fedha zitatolewa.
Maamuzi hayo yalitokana na hoja ya mbunge James Mbatia aliyetaka bunge liahirishe shughuli zake ili kujadili suala hilo kama jambo muhimu na la dharura.
Azzan alisema Kamati ya Uongozi ilikutana katika kikao cha pamoja na serikali pamoja na baadhi ya wabunge akiwemo James Mbatia na kukubaliana kwamba Tume ya Uchaguzi ikutane na Wadau wa zoezi hilo wiki ijayo wakiwemo Kituo cha Demokrasia Tanzania TCD kwa ajili ya kupata suluhu ya mchakato huo.
Alisema pia kuwa katika kikao hicho, kamati ya uongozi imeridhika na maelezo ya serikali kuhusu suala hilo na kuiagiza kamati ya Bunge ya Katiba Sheria na Utawala kulifuatilia suala hilo na kupeleka taarifa bungeni siku ya Ijumaa (Februari 6, 2015).
Hata hivyo taarifa hiyo ya mwenyekiti wa Bunge Musa Azzan haikusema ni kiasi gani na lini fedha zitatolewa.
Facebook Blogger Plugin by AllyTz
Post a Comment