Uchaguzi (NEC) imekabidhiwa jukumu la kuangalia utaratibu utakaotumika kuwezesha Watanzania walio nje ya nchi kushiriki kupiga kura katika Uchaguzi Mkuu unaofanyika Oktoba mwaka huu.


Taarifa hiyo ilitolewa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda wakati akijibu swali la Mbunge wa Mkanyageni, Habib Mnyaa (CUF) aliyetaka kufahamu maandalizi yaliyopo kwa ajili ya kuwezesha Watanzania waliojiandikisha walio nje ya nchi , kupiga kura.

Mnyaa katika swali la papo kwa hapo kwa Waziri Mkuu kuwa Tanzania ilisifiwa kukuza demokrasia kupitia Mwenyekiti wa Bunge Maalumu la Katiba aliporuhusu wabunge kupiga kura wakiwa nje ya nchi.

“ Kwa kuwa tuna uchaguzi wa Rais na Wabunge, na jambo hili linakwenda vizuri, je utaratibu gani au maandalizi gani yamefanyika ili Watanzania walioko nje ya nchi waliojiandisha waruhusiwe kupiga kura,” alisema Mnyaa.

Waziri Mkuu katika majibu, alisema ingawa Serikali ilishajaribu utaratibu huo siku zilizopita ikaonekana kuwapo matatizo ya kitaalamu, jambo hili limepelekwa NEC waone ni utaratibu gani utatumika kuwezesha walio nje ya nchi katika sehemu mbalimbali waweze kushiriki.
Alisisitiza kwamba anaamini Tume ya Uchaguzi itaona utaratibu mzuri ambao hautaleta kikwazo.

Facebook Blogger Plugin by AllyTz

Post a Comment

 
Top