Meneja  wa msanii wa muziki wa Bongo Fleva, Nasib Abdul ‘Diamond’, Babu Tale, amesema hawajawahi kupewa kiasi cha fedha Sh mil 500 na Waziri Mkuu mstaafu, Edward Lowassa, ili wampigie kampeni za urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM).
 
Babu Tale alisema hawawezi kukataa fedha nyingi kiasi hicho wakati wenyewe wanafanya muziki ili kupata fedha, hivyo hawajapewa kitu chochote.
 
Alisema  Diamond yupo tayari kumfanyia kampeni mgombea yeyote atakayetangazwa kuiwakilisha CCM katika uchaguzi mkuu mwaka huu. 
 

Meneja huyo alitoa ufafanuzi huo baada ya hivi karibuni kuzagaa kwa taarifa ambazo si za kweli, kwamba walipokea kiasi hicho ili kumpigia kampeni Lowassa.



Facebook Blogger Plugin by AllyTz

Post a Comment

 
Top