Marais watano wa nchi wanachama wa Jumuia ya Afrika Mashariki, Yoweri Museveni wa Uganda, Paul Kagame wa Rwanda, Pierre Nkurunzinza wa Burundi, Jakaya Kikwete wa Tanzania na mwenyeji wa mkutano Uhuru Kenyatta wa Kenya.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na mwenyeji wao Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya pamoja na Rais Yoweri Museveni wa Uganda, Rais Paul Kagame wa Rwanda na Rais Pierre Nkurunzinza wa Burundi wakizungumza chemba kabla ya kuingia kwenye ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa  Kenyatta International Convention Center(KICC)Nairobi,Kenya  katika mkutano wa kawaida wa 16 wa Wakuu wa nchi za Afrika Mashariki uliofanyika Ijumaa Februari 20, 2015 Rais Jakaya Mrisho Kikwete na mwenyeji wao Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya pamoja na Rais Paul Kagame wa Rwanda kwenye ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa  Kenyatta International Convention Center(KICC)Nairobi,Kenya  katika mkutano wa kawaida wa 16 wa Wakuu wa nchi za Afrika Mashariki uliofanyika Ijumaa Februari 20, 2015 Rais Jakaya Mrisho Kikwete, Naibu Rais wa Kenya, Mhe. William Rutto na maafisa wengine wakiwa kwenye ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa  Kenyatta International Convention Center(KICC)Nairobi,Kenya wakati wimbo wa Taifa wa Tanzania katika mkutano wa kawaida wa 16 wa Wakuu wa nchi za Afrika Mashariki uliofanyika Ijumaa Februari 20, 2015 Kutoka kushoto ni mgeni mwalikwa, Rais wa Sudani Kusini, Mhe Salva Kiir, Rais wa Burundi, Mhe Pierre Nkurunziza, Rais Jakaya Mrisho Kikwete(Tanzania),Rais Uhuru Kenyatta(Kenya)Rais Yoweri Museveni (Uganda) Rais Paul Kagame (Rwanda) na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) Balozi Dk Richard Sezibera wakiwa kwenye ukumbi wa mikutano kwenye  mkutano wa kawaida wa 16 wa Wakuu wa nchi za Afrika Mashariki Rais Jakaya Mrisho Kikwete(kushoto)akipokea bendera ya Afrika Mashariki(EAC)kutoka kwa Rais wa Kenya,Uhuru Kenyatta ikiwa ni ishara ya kumkabidhi rasmi Uenyekiti wa  EAC  kwenye  mkutano wa kawaida wa 16 wa Wakuu wa nchi za Afrika Mashariki uliofanyika Ijumaa Februari 20, 2015 katika ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Jomo Kenyatta jijini Nairobi. Picha na IKULU

***
Rais Jakaya Kikwete amekuwa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), akichukua jukumu hilo kutoka kwa Rais Uhuru Kenyatta aliyemaliza muda wake.

Makabidhiano hayo yalifanyika jana katika mkutano wa 16 wa wakuu hao wa nchi hizo uliofanyika kwenye Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Jomo Kenyatta.
 
Jana, nchi hizo zilizindua mfumo wa mawasiliano ya pamoja ambapo Rais Kikwete aliwasiliana na Balozi Sefue na kuzungumza naye mambo machache.
 
Marais wengine wa nchi hizo wanachama pia walifanya hivyo kwa kuwasiliana na mataifa yao.
 
Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki ilizindua mfumo huo ambao utaziwezesha nchi wanachama kupunguza gharama za uendeshaji wa mikutano baina ya wajumbe wao. 

Awali, wajumbe walilazimika kusafiri na kukutana sehemu moja.
 
Akielezea mfumo huo, Mkurugenzi Msaidizi wa Huduma za Jamii wa wizara hiyo, Eliabi Chodota alisema kuwa, utasaidia kupunguza gharama katika mikutano mbalimbali inayofanyika baina ya wajumbe wa nchi wanachama.
 
“Mfumo huu utaondoa haja ya wajumbe kukutana. Marais, mawaziri, makatibu wakuu pamoja na wafanyakazi wa Serikali wataendesha mikutano yao bila ya kukutana. Hii itapunguza matumizi ya fedha kwa ajili ya kujikimu na bajeti nyingine za mikutano,” alisema Chodota.
 
Alifafanua kuwa wanyakazi wa taasisi mbalimbali zinazoshirikiana wataweza kutatua matatizo yatakayojitokeza kwa kutumia mfumo huo jambo litakaloongeza ufanisi katika utatuzi wa kero ndogo ndogo zinazowakumba wananchi wa mataifa wanachama.
 
Awali, Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue alisema hafahamu sababu ya Kenya kuzuia magari yenye usajili wa Tanzania kufika na kuingia Uwanja wa Kimataifa wa Ndege wa Jomo Kenyatta nchini humo.
 
Balozi Sefue alisema hayo alipozungumza na gazeti hili katika ofisi za Wizara ya Afrika Mashariki (EAC), alikohudhuria uzinduzi wa mfumo wa kuendesha mikutano kwa njia ya video (video conferencing) uliokuwa ukifanyika Kenya.
 
Alisema Serikali inashangaa kuona zuio hilo linafanyika wakati mkataba wa ushirikiano katika sekta ya utalii baina ya nchi hizi mbili ulisainiwa mwaka 1985 na kubainisha vipengele vitakavyohusika.
 
“Mazungumzo yanaendelea ili kurekebisha tatizo lililojitokeza. Tumeshtushwa na zuio hilo licha ya kuwapo kwa mkataba unaoruhusu jambo hilo. Mpaka sasa hawajatuambia tatizo ni nini lililowafanya wazuie magari yetu,” alisema.
 
Katika hatua nyingine, suala la mgogoro huo wa kibiashara uliosababisha Kenya kuzuia magari maalumu ya watalii na abiria yenye namba za usajili za Tanzania kwenda Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta (JKIA) kushusha na kupakia abiria limefikishwa kwenye baraza la mawaziri wa kisekta wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) kwenye kikao kilichofanyika juzi jijini hapa.
 
Katika kikao hicho kilichoongozwa na mwenyekiti wa baraza la mawaziri wa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki, Dk Harrison Mwakyembe kilijadili mambo mbalimbali ya kisekta na mawaziri kutoka nchi za Rwanda, Burundi, Kenya, Tanzania na Uganda na nchi hizo mbili kuamua suala hilo linafaa kujadiliwa baina yao pekee yao.
 
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utali, Dk Adelhim Meru alithibitisha kikao hicho kufanyika na kusema hakikujadili mgogoro huo baada ya kukubaliana ujadiliwe baina ya nchi za Kenya na Tanzania katika mkutano utakaofanyika jijini Arusha, Machi 18 hadi 20 mwaka huu.
 
“Serikali zetu mbili zimeona ni busara tukawa na vikao vyetu wenyewe ambavyo kimsingi vilishaanza badala ya kuwashirikisha wanachama wengine wa EAC, ambao jambo hili haliwahusu moja kwa moja,” alisema Dk Meru.
 
Mgogoro huo ulianza Desemba mwaka jana baada ya Kenya kuyazuia magari ya Tanzania kufika moja kwa moja JKIA kupeleka abiria na kuwachukua kwa madai kuwa nchi hizo zina makubaliano ya mwaka 1985, inayozuia magari ya kitalii kutoingia kwenye vivutio vya kitalii vya nchi husika jambo ambalo Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu alilipinga kuwa viwanja vya ndege siyo sehemu za kitalii kwa mujibu wa makubaliano hayo.
 
Mmoja wa wafanyabiashara wa muda mrefu wa magari yanayofanya safari zake katika miji ya Nairobi na Arusha, James King’ori alisema utaratibu uliowekwa na Serikali ya Kenya umekuwa ukiwagharimu fedha zaidi kwani wanapofika sehemu waliyopangiwa hulazimika kukodi magari mengine ya kuwafikisha wageni wao uwanja wa ndege na kuwachukua waliowasili kwa utaratibu huo.
 
Waziri Nyalandu alisema inakadiriwa abiria 300,000 hutumia Uwanja wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta mjini Nairobi kuingia na kuondoka Tanzania kutokana na ubora wa miundombinu yake na wepesi wa kuunganisha safari katika nchi mbalimbali ulimwenguni.

Facebook Blogger Plugin by AllyTz

Post a Comment

 
Top